PROF.MUHONGO AMUENZI BABA WA TAIFA HAYATI MWALIMU NYERERE,AWACHANGIA VIJANA KATONI 200 ZA MAJI YA KUNYWA KWA AJILI YA MATEMBEZI YAO KUANZIA WILAYANI BUTIAMA MKOA WA MARA HADI MKOA WA MWANZA KATIKA KILELE CHA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2024 NA KUMBUKUMBU YA MIAKA 25 YA KIFO CHA MWALIMU NYERERE.

Leo tarehe 9.10.2024 Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Sospeter Muhongo amewatambelea vijana katika ufunguzi wa wiki yao Kitaifa uliofanyika Wilaya ya Butiama Mkoani Mara.

Katika hatua nyingine Prof.Muhongo amepata nafasi ya kuwasalimia vijana hao na kumuelezea kwa kifupi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika historia ya ujenzi wa Taifa la Tanzania na Chama cha Mapinduzi CCM.
Pia amewachangia katoni 200 za maji ya kunywa vijana hao zidi ya 600 ili ziwasaidie njiani katika kumuenzi Baba wa Taifa wakielekea Mkoani Mwanza.

Katika uzinduzi huo Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Bi.Rehema Sombi alikuwa Mgeni Rasmi akiongozana na Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Bi Jokate Mwegelo.

Tunazima zote tunawasha kijani.