MASHINDANO YA KUPIGA KASIA 2019 (THE ANNUAL BOAT RACE)

VIKOMBE vya WASHINDI na T-SHIRT za Washiriki

Jumapili, 29.12.2019
Jimbo la Musoma Vijijini

KIPAUMBELE Na. 5 (Michezo na Utamaduni) cha Jimbo la Musoma Vijijini kinaendelea kutekelezwa na kesho, Jumatatu, 30.12.2019 kuna MASHINDANO YA KUPIGA KASIA Kijijini Bukima, Kata ya Bukima.

MASHINDANO hayo, kama yalivyo ya KWAYA (Nyimbo), NGOMA za ASILI na MPIRA wa MIGUU ni sehemu ya UTEKELEZAJI wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2015-2020, ndani ya Jimbo letu (Rejea Kitabu cha Kurasa 110 cha Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani hiyo: Januari 2016 – Juni 2019, Jimbo la Musoma Vijijini).

Matayarisho ya MASHINDANO hayo yamekamilika.

MAHALI:
Mwalo (Ufukwe) wa Kijiji cha Bukima

SIKU:
Jumatatu, 30.12.2019

MUDA:
Timu zinazoshindana zitawasili MWALONI (ufukweni) Bukima Saa 2.30 Asubuhi

UKUBWA WA TIMU:
Wapiga kasia 5 kwa kila MTUMBWI (Timu)

USALAMA:
Taratibu za usalama majini (ziwani) zitazingatiwa.

KATA ZILIZOJIANDIKISHA kushiriki kwa ridhaa zao:

(1) Bugwema, (2) Bukima, (3) Bukumi, (4) Bwasi, (5) Etaro, (6) Mugango, (7) Murangi, (8) Musanja, (9) Nyakatende, (10) Rusoli na (11) Suguti

ZAWADI KWA WASHINDI

*Mshindi wa 1
Tsh Milioni 1 & Kikombe

*Mshindi wa 2
Tsh 700,000 & Kikombe

*Mshindi wa 3
Tsh 400,000 & Kikombe

*Kifuta jasho kwa WASHIRIKI ambao hawatashinda: Tsh 50,000 kwa Timu.

SIKUKUU YA KRISMASI KIJIJINI NYASAUNGU – WANAKIJIJI WASISITIZA SEKONDARI YAO KUFUNGULIWA MWAKANI (2020)

Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo akiendesha HARAMBEE ya ujenzi wa Nyasaungu Secondary School

SHEREHE YA KRISMASI Jimbo la Musoma Vijijini imetumika kuboresha UAMUZI  wa Wananchi wa Kijiji cha Nyasaungu wa kuhakikisha SEKONDARI MPYA inayojengwa Kijijini mwao INAFUNGULIWA Mwakani (Februari 2020).
SHEREHE za Eid al Fitr, Krismasi na Pasaka za Jimbo la Musoma Vijijini zinafanywa kwa mzunguko ndani ya Kata zote 21 za Jimbo hili.
Marafiki 2 (na wanafunzi wenzake) wa  Prof Muhongo wa kutoka Jijini Berlin,  Ujerumani (Magharibi) walihudhuria SHEREHE hiyo. Hao ni: Christa Werner (Dr.rer.nat.) na Wolfgang Zils (Dipl Ing, Dipl Geol).
Jimbo la Musoma Vijijini lina Jumla ya Kata 21. Kata 18 tayari zilishajenga Sekondari zao na zinatumika. Kata 3 (Bugoji, Busambara na Ifulifu) zisizokuwa na Sekondari zinakamilisha ujenzi wa Sekondari zao ili zianze kutumika mwakani (2020).
Kwa hiyo, ifikapo Februari 2020 KILA KATA Jimboni itakuwa inayo Sekondari yake. Kutokana na WINGI wa Wanafunzi na UMBALI wa kutembea, baadhi ya Kata zimeanza kujenga Sekondari ya pili kwenye Kata zao. Jumla ya Sekondari za Binafsi Jimboni ni mbili (2).
HARAMBEE YA KRISMASI – Nyasaungu Secondary School
Baada ya Ibada ya Krismasi, Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo aliendesha HARAMBEE ya kuchangia VIFAA VYA ujenzi vitakavyotumika ifuatavyo:
*Vyumba 3 vya Madarasa viezekwe ifikapo tarehe 15.1.2020
*Vyoo vya Wanafunzi  na Walimu vikamilishwe ujenzi wake kabla ya tarehe 30.1.2020
MFUKO wa JIMBO ulishachangia MABATI 54 ya kuezeka chumba kimoja cha darasa.
Tarehe 25.12.2019, Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo alichangia MABATI 54. Hapo awali, Mbunge huyo alishachangia SARUJI MIFUKO 35 na NONDO 20 kwa ajili ya ujenzi wa Sekondari hii.

KRISMASI 2019 – WANAVIJIJI WAFURAHIA ZAWADI YA MAJENBE YA KUKOKOTWA NA NG’OMBE (PLAU)

UTOAJI wa ZAWADI YA KRISMASI ya PLAU kwa VIKUNDI 20 vya KILIMO vya Jimbo la Musoma Vijijini

VIKUNDI 20 VYA KILIMO kutoka VIJIJI 20 ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini WAMEPOKEA KWA FURAHA KUBWA Zawadi ya Krismasi kutoka kwa Mbunge wao, Prof Sospeter Muhongo.
ZAWADI hiyo iliyotolewa tarehe 24.12.2019 kwa kila Kikundi ni PLAU MOJA – Jembe la kukokotwa na ng’ombe moja. Mbunge huyo AMETOA ZAWADI hiyo ikiwa ni ISHARA ya kuanza rasmi KAMPENI ya kupunguza matumizi ya JEMBE la MKONO Jimboni humo.
PLAU hizo zimegawiwa kwenye Vituo 2:
KITUO 1: CHUMWI SENTA – Vikundi kutoka Vijiji vya:
Bukima, Butata, Chimati, Chitare, Chumwi, Mabui Merafuru, Masinono, Mikuyu, Kaburabura, Rusoli, Suguti na Wanyere
KITUO 2: NYASURURA SENTA – Vikundi kutoka Vijiji vya: Kamguruki, Kwibara, Maneke, Mwiringo, Nyakatende, Nyasaungu, Nyegina na Tegeruka.
MADIWANI na Viongozi wengine wa Kata zenye Vijiji vilivyopewa ZAWADI hiyo ya KRISMASI walikuwepo.
Mbunge wa Jimbo aliambatana na rafiki zake wa miaka mingi kutoka Ujerumani ambao wamemtembelea huko Jimboni. Wageni hao, Christa Werner (Dr.rer.nat.) na Wolfgang Zils (Dipl Ing, Dipl Geol) walisoma na Prof Muhongo huko Ujerumani ya Magharibi miaka ya 80.
KRISMASI YA JIMBO (2019)
Itafanyika Kijijini Nyasaungu, Kata ya Ifulifu.
HARAMBEE ya ujenzi wa Nyasaungu Secondary School, IBADA KANISANI na Chakula cha Mchana cha Krismasi (CHRISTMAS LUNCH), vyote vimefanyika Kijijini Nyasaungu,  tarehe 25.12.2019.

VIKUNDI VYA KILIMO KUPEWA ZAWADI YA KRISMASI YA KUBORESHA KILIMO CHAO

Wakulima wa Vijiji vya Bukumi (Kata ya Bukumi) na Kamuguruki (Kata ya Nyakatende) wakiwa mashambani mwao, kwenye Kilimo cha MSIMU huu (2019/2020), kwa kutumia MAJEMBE ya KUKOKOTWA na NG’OMBE (PLAU).

Na: Fedson Masawa
Msaidizi wa Mbunge
Zimebaki siku 2 kabla Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo kukabidhi ZAWADI ya KRISMASI ya PLAU (Majembe ya kukokotwa na Ng’ombe) kwa VIKUNDI VYA KILIMO 18 vya Wakulima ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.
WAKULIMA Jimboni wanaendelea kuhamasika zaidi kwa kutambua umuhimu wa kutumia PLAU (na MATREKTA yakipatikana) badala ya JEMBE LA MKONO.
WAKULIMA wameeleza kuwa, tofauti na kipindi cha nyuma, ambacho Wakulima wengi walikuwa wakitumia Majembe ya Mkono  kwenye kilimo chao, kwa sasa Wakulima walio na MAJEMBE ya NG’OMBE (PLAU) wanatumia majembe hayo kulima eneo kubwa kwa muda mfupi.
Ndugu Majura Mbogora wa Kijiji cha Bukumi ameeleza kwamba Mkulima anaweza kulima EKARI MOJA kwa siku moja kwa kutumia PLAU MOJA wakati kulima shamba hilo hilo kwa kutumia JEMBE la MKONO, siku 5  hadi 7 zinahitajika kwa Familia ya watu wasiopungua watano (5). Hivyo, WAKULIMA wanaona kuna umuhimu wa KULIMA kwa kutumia PLAU ili kupanua ukubwa wa mashamba yao kwa kutumia muda mfupi zaidi.
ZAWADI ZA PLAU KWA VIKUNDI VYA KILIMO
Tarehe 24.12.2019, Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo atatoa ZAWADI YA KRISMASI YA PLAU kwa kila KIKUNDI cha KILIMO kutoka VIJIJI 18. Hii ni sehemu ya KAMPENI ya KUSHAWISHI Wakulima wapunguze kutumia JEMBE la MKONO na waanze kutumia PLAU kwa wingi.
VIONGOZI wa VIKUNDI vya KILIMO 18 vitakavyopewa ZAWADI YA PLAU kwa kila KIKUNDI wanatanguliza SHUKRANI zao za DHATI kwa Mbunge wa Jimbo lao kwa KUENDELEA KUBORESHA KILIMO Jimboni mwao.
Vilevile, WAKULIMA wanamshukuru sana Mbunge wao kwa kuwagawia bure MBEGU za mazao ya ALIZETI, MIHOGO, MTAMA na UFUTA kwa misimu kadhaa ya kilimo chao.
MATREKTA YA MKOPO
Jimbo la Musoma Vijijini lina jumla ya Vyama vya Ushirika vya Msingi vya Mazao (AMCOS) 35. Idara ya Kilimo ya Halmashauri (Musoma DC) yenye Jimbo hili IKO TAYARI kusaidia AMCOS hizo kutayarisha nyaraka za kutafuta MIKOPO ya kununua MATREKTA kwa manufaa ya Wanachama wao.

JUBILEE YA SHULE YA MSINGI MWIRINGO YAFANA NA WANANCHI WAAHIDI KUONGEZA KASI KWENYE UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO YAO

Burudani kutoka kwa Wanafunzi wa S/M Mwiringo katika kusherehekea Jubilee ya shule yao

WANANCHI wa Kijiji cha Mwiringo, Kata ya Busambara WAMEJIWEKEA MALENGO MAPYA YA KUONGEZA KASI YA MAENDELEO YAO:
* Wataongeza kasi ya USHIRIKIANO wao na Serikali kutekeleza Miradi ya Maendeleo kijijini mwao na kwenye Kata yao.
* Wataendelea KUBORESHA MIUNDOMBINU ya Shule ya Msingi Mwiringo. Wameanza kwa kuchanga fedha za kukamilisha ujenzi wa Vyumba 2 vya Madarasa na Ofisi ya Walimu.
* Wamechanga fedha za kukamilisha ujenzi wa Vyoo vya Wavulana kwenye SEKONDARI MPYA ya Kata yao (Busambara Secondary School). Ujenzi wa Vyoo hivyo utakamilika ifikapo tarehe 24.12.2019.

ZAO LA DENGU LAANZA KULIMWA KWENYE BONDE LA BUGWEMA

Ndugu Owiyo na Familia yake wakiwa kwenye palizi ya DENGU. Hapo ni Kijijini Masinono, Kata ya Bugwema.

Jumapili, 15.12.2019
Jimbo la Musoma Vijijini
Na: Hamisa Gamba
Msaidizi wa Mbunge
KATA ya BUGWEMA inayoundwa na Vijiji vinne (4) yaani Muhoji, Masinono, Kinyang’erere na Bugwema ina BONDWE kubwa kwa ajili ya Kilimo cha Mazao ya CHAKULA na BIASHARA. Kilimo kikubwa cha UMWAGILIAJI kitatekelezwa kwenye BONDE hili.
Bonde la BUGWEMA lina ukubwa wa EKARI 5,075 (hekta 2,054)
Mazao makuu ya CHAKULA yanayolimwa BUGWEMA ni: MAHINDI, MIHOGO, MTAMA, MPUNGA, VIAZI VITAMU, MATUNDA na MBOGAMBOGA.
Mazao Makuu ya BIASHARA yanayolimwa BUGWEMA ni: PAMBA, ALIZETI, MPUNGA, MAHINDI na DENGU.
DENGU ni zao JIPYA la CHAKULA na BIASHARA liloanzwa kulimwa BUGWEMA kwa miaka ya karibuni. Ni moja ya MAZAO yatakayoendelea kulimwa kwa wingi kwenye BONDE la BUGWEMA kwenye KILIMO CHA UMWAGILIAJI kitakachoendeshwa na MRADI mkubwa wa Benki ya Kilimo (Tanzania Agricultural Development Bank, TADB) kwa kushirikiana na WANAVIJIJI na HALMASHAURI ya Wilaya ya Musoma (Musoma DC). Mazao mengine ya MRADI huo ni: MPUNGA, VITUNGUU, MAHINDI, ALIZETI na PAMBA.
Mmoja ya Wakulima wa DENGU kwenye Kijiji cha Masinono, Ndugu Francis Owiyo  amesema kwamba hivi karibuni ameanza kujishughulisha na Kilimo cha DENGU. Vilevile, hulima ALIZETI. Ndugu Owiyo ambaye kwa sasa ameanza kwa kulima Ekari 3 za DENGU, amesema  kuwa zao hilo kwa  kawaida linachukua takribani miezi mitatu  (3) kuwa tayari kwa kuvunwa.
Mkulima huyo amesema KILO 1 ya DENGU huuzwa kwa bei ya Shilingi 800 – 1,000. Ndugu Owiyo anasubiri kwa hamu kubwa MRADI wa Kilimo cha UMWAGILIAJI kwenye BONDE la BUGWEMA. Anakusudia kupanua mashamba yake kwa kutumia ZANA za KISASA za KILIMO zitakazotolewa na Benki ya Kilimo (TADB).
Diwani wa Kata ya Bugwema, Mhe Ernest Magembe ameendelea kushawishi na kushauri wananchi wa Kata hiyo kuhakikisha wanaongeza juhudi kubwa kwenye Kilimo ili kutokomeza NJAA kwenye Kata yao na Jimboni kwa ujumla.
Diwani huyo ameendelea kutoa shukrani za pekee kwa Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo kwa kugawa bure mbegu za MTAMA, MIHOGO, UFUTA na ALIZETI kwa Wakulima wa Kata ya Bugwema na Jimboni kote (Kata 21).
Diwani huyo ameongeza kwa kusema kwamba Wanavijiji wa Kata ya Bugwema ndio WAKULIMA MASHUHURI wa mazao ya ALIZETI na DENGU ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.
HATUTAKI NJAA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – TWENDENI SHAMBANI!

MAZAO YA VIKUNDI VYA KILIMO YAPATA KWA URAHISI MASOKO YA NDANI

Kikundi cha NO SWEAT NO SWEET wakiwa na mavuno yao ya MATIKITI. Mfanyabiashara, Ndugu Salha Mohamed ameenda Kijijini Bwasi kununua MATIKI ya Kikundi hicho.

Jumapili, 8.12.2019
Na: Verediana Mgoma
Msaidizi wa Mbunge
KIKUNDI cha NO SWEAT NO SWEET cha Kata ya Bwasi kinaendelea kunufaika na MRADI wa KILIMO baada ya kujifunza kulima mwaka mzima, yaani kwa vipindi vya kiangazi na masika.
Mwenyekiti wa KIKUNDI hiki, Ndugu Goodluck Wambwe ameeleza kuwa wako kwenye KILIMO cha BIASHARA cha Mazao ya MAHINDI, MATIKITI, VITUNGUU na NYANYA.
Kiongozi huyo ameongeza na kusema kwamba, WAMEFANIKIWA KUNUNUA MASHINE YA PILI ya Umwagiliaji.
Vilevile, KIKUNDI hiki KIMEFANIKIWA kufungua AKAUNTI BENKI, kununua SHAMBA jingine, kulipa ADA za masomo ya watoto wao na kuhudumia FAMILIA zao kwa ubora zaidi.
Ndugu Salha Mohamed (pichani), Mfanyabiashara kutoka Kijiji cha Bukima anashukuru sana kwa VIKUNDI vya KILIMO hasa vya UMWAGILIAJI kujitokeza kwa wingi JIMBONI humo na  kulima MAZAO ya BIASHARA.
“Kwa sasa tumepunguza sana gharama za kusafiri nje ya Jimbo letu kwenda kununua MAZAO ya BIASHARA. Bidhaa nyingi tunazipata ndani ya Jimbo letu”, alisema Mfanyabiashara huyo, Ndugu Salha Mohamed.
Ndugu Gustavu Tesha, Kaimu Afisa Kilimo wa Kata ya Bwasi amekuwa akitoa elimu juu ya KILIMO cha UMWAGILIAJI na kufanikiwa kuongeza idadi ya VIKUNDI vya KILIMO cha  UMWAGILIAJI ndani na nje ya Kata hiyo.
Wanachama na Viongozi wa Kikundi cha NO SWEAT NO SWEET wanamshukuru sana Mbunge wao  Profesa Sospeter Muhongo kwa kuwapatia MASHINE ya kwanza ya UMWAGILIAJI. Hiki Kikundi ni moja ya VIKUNDI 15 vilivyopewa MASHINE za UMWAGILIAJI na mbegu Mwaka 2016. Vifaa hivi vilinunuliwa kutoka kwenye Fedha za MFUKO wa JIMBO.
VIKUNDI VYA KILIMO CHA UMWAGILIAJI vinazidi kuongezeka ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.
Tarehe 24.12.2019 (Christmas Eve) Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo ATATOA ZAWADI YA KRISMASI ya PLAU (jembe la kukokotwa na ng’ombe) kwa VIKUNDI 14 kutoka VIJIJI 14 vya Jimbo la Musoma Vijijini.

BARAZA LA MADIWANI LAFANYA UAMUZI WA KUJENGA VETA KWENYE HALMASHAURI YAO

Wajumbe wa BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Kikao kilifanyika tarehe (6.12.2019) kwenye Ukumbi wa Kanisa Katoliki Mugango.

BARAZA la MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma  LIMEFANYA UAMUZI MUHIMU kwa Maendeleo ya Wananchi wa Halmashauri hiyo yenye Jimbo la Musoma Vijijini.
JIMBO hilo lina Kata 21, Vijiji 68 na Vitongoji 374.
Shule za Msingi za Serikali ni 111, za Binafsi ni 3 na Shule Shikizi ni 10. Jimbo lina Sekondari za Serikali/Kata 18, za Binafsi 2 na Sekondari Mpya zinazojengwa ni 9. WINGI wa WAHITIMU wa Shule zote hizi WANAHITAJI FURSA ZAIDI za kujiendeleza kiuchumi.
WILAYA ya Musoma yenye Jimbo la Musoma Vijijini na Jimbo la Musoma Mjini inayo VETA MOJA iliyoko Musoma Mjini. Kwa hiyo UAMUZI wa leo (6.12.2019) wa BARAZA la MADIWANI wa Jimbo la Musoma Vijijini UNASTAHILI PONGEZI NYINGI sana – KUPANUA WIGO WA FURSA ZA  WAHITIMU kujiendeleza kiuchumi.
VETA itakayojengwa itazingatia hali halisi ya Sekta Kuu za Uchumi (k.m. Uvuvi, Kilimo na Ufugaji) wa Jimbo la Musoma Vijijini.

WANAVIJIJI WATATHMINI MAENDELEO YA VIJIJI VYAO YA MWAKA HUU (2019)

KIKAO cha tarehe 4.12.2019 cha Viongozi wa MABARAZA ya WAZEE kijijini Suguti. TATHMINI za WANAVIJIJI za UCHUMI na MAENDELEO ya VIJIJI vyao kwa MWAKA huu (2019) ziliwasilishwa.

Jumatano, tarehe 4.12.2019, VIONGOZI wa MABARAZA ya WAZEE ya Ushauri, Ushawishi, Utamaduni na Maadili ya VIJIJI waliwasilisha TATHMINI za MIRADI YA UCHUMI na MAENDELEO ya VIJIJI vyao.
KIKAO hicho kilifanyika Kijijini SUGUTI chini ya Uenyekiti wa Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo.
TATHMINI za Vijiji zimewasilishwa na Mwenyekiti na Katibu wa Baraza la kila Kijiji. Jimbo lina Kata 21 na Vijiji 68. KIKAO cha VIONGOZI wa MABARAZA ya KATA kitakafanyika baadae.
TATHMINI zilifanyika kwenye SEKTA za: (i) Elimu, (ii) Afya, (iii) Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, (iv) Mazingira na (v) Michezo na Utamaduni. Vilevile, TATHMINI zimeongelea MIRADI ya maji, umeme, barabara, vyombo vya  usafirishaji na mawasiliano.
MAAZIMIO:
Baada ya uwasilishi na mjadala kukamilika, yafuatayo ni MAAZIMIO yatakayofikishwa Vijijini kwa UTEKELEZAJI:
(1) Hakuna Wanafunzi kusomea CHINI ya MITI. Kila Shule kijijini iwe na Vyumba vya Madarasa ya kutosha. MABARAZA yatashawishi na kushauri kazi hii ikamilike ifikapo 30 Juni 2020.
(2) MABARAZA yatashawishi na kushauri UPANDAJI wa MITI kwa WINGI kwa kila Kijiji. MICHE ya BURE inapatikana kwa Mkuu wa Wilaya (DC) ya Musoma.
(3) MABARAZA yatashawishi na kushauri Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu kuunda VIKUNDI vya UCHUMI na kuomba MIKOPO kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Musoma yenye Jimbo la Musoma Vijijini.
(4) MABARAZA yatashawishi na kushauri WAKULIMA na WAFUGAJI kuunda VIKUNDI VYA KILIMO vya kutumia PLAU (majembe ya kulimia yanayokokotwa na ng’ombe).
ZAWADI YA KRISMASI YA PLAU KWA VIKUNDI VYA KILIMO
Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo ATATOA ZAWADI YA PLAU (tarehe 24.12.2019) kwa VIKUNDI VYA KILIMO vilivyokuwa vya kwanza kuundwa na kuanza kazi.
VIKUNDI hivyo vinatoka Vijiji (14) vya: Bukima, Butata, Chitare, Chumwi, Kamguruki, Kwibara, Mabui Merafuru, Nyakatende,  Nyegina, Mikuyu, Rusoli, Suguti, Tegeruka na Wanyere.

SEMINA ELEKEZI NA MIKOPO ISIYOKUWA NA RIBA YA TSH 116.5 MILIONI VYATOLEWA KWENYE HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA (MUSOMA DC)

Jumatatu, tarehe 2.12.2019 HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA yenye Jimbo la Musoma Vijijini ILITOA SEMINA ELEKEZI kwa WENYEVITI WAPYA wa Vijiji juu ya UENDESHAJI WA SERIKALI ZA VIJIJI.
SEMINA hiyo imehudhuriwa na Wenyeviti 64 kati ya 68 (Mahudhurio 94.12%, Wenyeviti 4 wameomba udhuru).
Baadhi ya masuala muhimu yaliyotolewa MAFUNZO ni juu ya: Sheria ya Serikali za Mitaa, Muundo wa Serikali (Halmashauri) ya  Kijiji, Kamati za Halmashauri ya Kijiji na Majukumu yake, Vikao/Mikutano (Wajumbe wake na Kazi zake), Utungaji wa Sheria ndogo ndogo za Kijiji, Vyanzo vya Mapato, Majukumu ya Mwenyekiti, Taratibu za kumuondoa madarakani Mwenyekiti wa Halmashauri wa Kijiji, n.k. Fursa iliyotolewa ya KUULIZA MASWALI.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Musoma Vijijini, Ndugu Nyabukika Bwire Nyabukika ALIKARIBISHWA kutoa salamu za CHAMA kwa WENYEVITI hao. MGENI RASMI alikuwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo.
SEMINA ELEKEZI kwa WENYEVITI wa VITONGOJI 374 wa Halmashauri hii itatolewa siku chache zijazo.
TSH 116.5 MILIONI – MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WATU WENYE ELEMAVU, VIJANA NA WANAWAKE
Halmashauri ya Wilaya ya Musoma chini UONGOZI WENYE UBUNIFU MKUBWA wa Mkurugenzi Mtendaji (DED), Ndugu John Kayombo, leo (2.12.2019) IMETOA MIKOPO YA TSH MILIONI 116.5 kwa Makundi hayo matatu.
IKUMBUKWE kwamba hii ROBO YA KWANZA YA MWAKA WA FEDHA wa 2019/2020 na tayari HALMASHAURI hii INATEKELEZA KWA VITENDO UTOAJI wa MIKOPO kama ilivyoagizwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2015-2020.
*MIKOPO KWA WATU WENYE ULEMAVU
Vikundi 3 vyenye Jumla ya Wanachama 45 vimepewa Jumla ya  Tsh Milioni 15. Vikundi hivyo vinatoka Vijiji vya Bukima, Murangi na Nyambono.
*MIKOPO KWA VIKUNDI VYA VIJANA
Vikundi 4 vyenye Jumla ya Wanachama 78 vimepewa Jumla ya Tsh Milioni 21. Vikundi hivyo vinatoka Vijiji vya Lyasembe, Maneke, Kataryo na Kisiwa cha Rukuba.
*MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANANAWAKE
Vikundi 16 vyenye Jumla ya Wanachama 285 vimepewa Jumla ya Tsh Milioni 80.5. Vikundi hivyo vinatoka Vijiji vya Murangi (3), Tegeruka (2), Kwikuba (2), Bukima (1), Bujaga (1),  Saragana (1), Kwibara (1), Kataryo (1), Bwai Kwitururu (1), Busungu (1), Mayani (1) na Kome (1). MGENI RASMI alikuwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo.
Utoaji wa MIKOPO ISIYOKUWA NA RIBA ni endelevu. Vipo VIKUNDI vilivyopewa Mikopo Mwaka wa Fedha wa 2018/2019 na vingine BADO VITAPEWA mikopo ndani ya Mwaka huu wa Fedha (2019/2020)
WENYEVITI wa Serikali ya Vijiji, VIKUNDI vilivyopokea MIKOPO isiyokuwa na RIBA, na VIONGOZI mbalimbali Waliohudhuria shughuli hizi mbili WAMETOA SHUKRANi nyingi za dhati kwa Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt John Pombe Joseph Magufuki na Viongozi wengine wa Chama na Serikali kwa kuunga mkono juhudi za Wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini kwenye Utekelezaji wenye MAFANIKIO MAKUBWA wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2015-2020) ndani ya Jimbo lao.

KUANZA KWA MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA LAMI YA MUSOMA-MAKOJO- BUSEKELA

kazi zinazoendelea kwenye ujenzi wa Barabara ya LAMI ya Musoma-Makojo-Busekela

AHADI ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt John Pombe Joseph Magufuli yaanza kutekelezwa kwenye Jimbo la Musoma Vijijini. Mhe Rais alitoa AHADI hii wakati wa Kampeni za UCHAGUZI wa 2015 akiwa Kijijini Kabegi, Kata ya Ifulifu.
BARABARA ya Musoma-Makojo-Busekela yenye urefu wa kilomita 92 imeanza KUJENGWA kwa kiwango cha LAMI. Ujenzi umeanzia kwenye LOT II (Kusenyi-Makojo -Busekela). LOT I ni Musoma-Mugango-Kusenyi.
Kuanza kwa MRADI wa ujenzi wa Barabara hii muhimu sana kwa UCHUMI na MAENDELEO ya Wilaya ya Musoma ni kielelezo na kithibitisho kingine cha MAFANIKIO ya UTEKELEZAJI wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2015-2020 ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.
Jimbo la Musoma Vijijini lenye Kata 21, Vijiji 68 na Vitongoji 374 linajishughulisha na KILIMO (mazao makuu: mihogo, mahindi, mpunga, viazi vitamu, matunda, mbogamboga,  pamba na alizeti), UVUVI (sangara, sato, dagaa, n.k.), UFUGAJI (ng’ombe, mbuzi, kondoo na kuku) na UCHIMBAJI MADINI (dhahabu).
Kwa hiyo BIDHAA za aina mbalimbali za kutoka Musoma Vijijini zitafika kwa uharaka na ubora wake kwenye MASOKO tarajiwa.
WANANCHI na VIONGOZI wa Wilaya ya Musoma yenye Jimbo la Musoma Vijijini WANAENDELEA kutoa SHUKRANI zao za DHATI kwa Mhe Rais wao, Mhe Dkt John Pombe Joseph Magufuli kwa kutimiza AHADI aliyoitoa Jimboni mwao – ujenzi wa barabara ya LAMI.