MICHANGO INAHITAJIKA ILI SEKA SEKONDARI IFUNGULIWE JANUARI 2021

Baadhi ya MABOMA ya SEKA SEKONDARI yanayopaswa kukamilishwa kabla ya tarehe 30.12.2020 – UNAKARIBISHWA SANA UCHANGIE ujenzi huu

KATA ya NYAMRANDIRIRA ina Vijiji 5 (Chumwi, Kaboni, Kasoma, Mikuyu na Seka) na Sekondari moja, KASOMA SEKONDARI. Sekondari hii imeelemewa na WINGI wa WANAFUNZI wa kutoka Vijiji 5 WANAORUNDIKANA madarasani.

Baadhi ya Wanafunzi hao wanatembea UMBALI MREFU wa zaidi ya kilomita 10 kwenda masomoni kwenye Sekondari hiyo.

SULUHISHO: kujenga Sekondari ya pili ya Kata hiyo. Ujenzi umeanza na lengo kuu ni kuifungua mwakani (Januari 2021).

MAJENGO YANAYOJENGWA KWA SASA

* Vyumba 8 vya Madarasa
* Jengo la Utawala
* Vyoo vya Wanafunzi & Walimu
* Maabara
* Maktaba
* Nyumba za Walimu

MAJENGO YANAYOHITAJIKA KWA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA MWAKANI

IDADI YA WANAFUNZI:

* Maoteo: Wanafunzi 250 wa Kata ya Nyamrandirira watafaulu kujiunga na Kidato I mwakani, Januari 2021

* Maoteo: Wanafunzi 100 watajiunga na SEKA SEKONDARI

* Wanafunzi 150 watajiunga na KASOMA SEKONDARI

MAJENGO YANAYOPASWA KUKAMILISHWA KABLA YA TAREHE 30 DISEMBA 2020:

(1) Vyumba 3 vya Madarasa
(2) Ofisi 1 ya Walimu
(3) Choo chenye Matundu 8

WANAOCHANGIA UJENZI HUU (hadi leo hii):

(1) Wanavijiji wa Vijiji 5
(2) Viongozi wa Vijiji/Kata
(3) Mgodi Mdogo wa Dhahabu wa Seka
(4) Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo (alishachangia Saruji Mifuko 150)

MABATI 54:
Tarehe 24.11.2020, Mbunge wa Jimbo, Prof S Muhongo atachangia MABATI 54 ya kuezeka Chumba 1 cha Darasa.

WAZALIWA WA KATA YA NYAMRANDIRIRA:
* Wanavijiji bado wanasubiri kwa shauku kubwa AHADI za MICHANGO ya WAZALIWA (na marafiki zao) wa Kata hiyo.

MICHANGO IPELEKWE kwa:
* Mtendaji: 0756 680 887
* DC wa Wilaya ya Musoma
* Mkurugenzi wa Halmashauri (Musoma DC)

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz