HUDUMA ZA AFYA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

Ukubwa wa Jimbo letu:
Kata 21 zenye vijiji 68 na vitongoji 374

Idadi ya hospitali, vituo vya afya na zahanati:

(1) Hospitali ya Halmashauri/Wilaya inayotoa Huduma za Afya (1)
+Imejengwa Kitongoji cha Kwikonero, Kijiji cha Suguti, Kata ya Suguti

(2) Vituo vya Afya vya Kata vinavyotoa Huduma za Afya (3):
(i) Kijijini Murangi, Kata ya Murangi
(ii) Kijijini Nyang'oma, Kata ya Mugango
(iii) Kijijini Bwai Kwitururu, Kata ya Kiriba

(3) Vituo vya Afya vya Kata vinavyosubiri kufunguliwa, vifaa vya matibabu vimeanza kupelekwa (3):
(i) Kijijini Makojo, Kata ya Makojo
(ii) Kijijini Masinono, Kata ya Bugwema
(iii) Kisiwani Rukuba, Kata ya Etaro

(4) Zahanati zinazotoa Huduma za Afya:
(i) 26 za Serikali
(ii) 4 za Binafsi

(5) Zahanati zinazojengwa kwa kutumia michango ya wanavijiji na wadau wao wa maendele ni 17

Baadhi ya zahanati hizi zimeanza kupokea michango ya fedha kutoka Serikalini - tunashukuru sana

Orodha yake inawekwa hapa ili kukaribisha michango kutoka kwa Wadau wetu wa Maendeleo, wakiwemo Wazaliwa wa Musoma Vijijini.

Ujenzi unafanyika ndani ya vijiji 17:
Bulinga, Burungu, Butata, Chanyauru, Chimati, Chirorwe, Kaburabura, Kakisheri, Kataryo, Kwikerege, Kurukerege, Kurwaki, Mabuimerafuru, Maneke, Nyabaengere, Nyambono na Nyasaungu

Picha iliyoambatanishwa hapa inaonesha:
Ujenzi wa boma la zahanati ya Kijiji cha Kataryo, Kata ya Tegeruka

ILANI YA UCHAGUZI YA CCM YA MWAKA 2020-2025 INATEKELEZWA VIZURI SANA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI - karibuni tuchangie ujenzi wa zahanati mpya vijijini mwetu.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
Jumamosi, 13.7.2024