Leo, Ijumaa, 11.10.2024, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo, amejiandikisha kupiga kura tarehe 27.11.2024.

Vilevile, ametembelea vitongoji kadhaa vya Kata nne, ikiwemo Kata ya kwao ya Kiriba, yenye vijiji 3 na vitongoji 24, na kupata yafuatayo:

(i) Idadi ya wapiga kura waliojiandikisha ndani ya Kata ya Kiriba kwa siku ya leo: 1,856

(ii) Idadi ya wapiga kura waliojiandikisha kwenye Kitongoji cha Miembeni (Kituo cha Afya), Kijiji cha Bwai Kwitururu
Kufikia saa 6 mchana: 22
Kufikia saa 12 jioni: 50
Prof Sospeter Muhongo amejiandikisha hapo

Uhamasishaji:
Wananchi waendelee kuhamasishwa kujitokeza kujiandikisha kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa tarehe 27.11.2024

Picha zilizoambatanishwa hapa zinaonesha:

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo, akijiandikisha kupiga kura, na kutembelea vituo kadhaa vya uandikishaji wapiga kura ndani ya kata nne za Musoma Vijijini.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
Ijumaa, 11.10.2024