Kisiwa cha Rukuba kilitambuliwa na kupewa hadhi ya kijiji Mwaka 1974.

Kisiwa hiki ni moja ya vijiji vinne (4) vya Kata ya Etaro. Vijiji vingine ni: Busamba, Etaro na Mmahare.

Baadhi ya mafanikio yaliyopatikana ndani ya Miaka 50 ya Kisiwa cha Rukuba:

(1) kuwepo kwa Shule ya Msingi yenye vyumba vya madarasa vya kutosha na madawati ya kutosha.

(1a) Shule ina Ofisi mbili (2) za Walimu (Mwalimu Mkuu & Walimu wengine)

(2) kuwepo kwa Maktaba ya Shule ya Msingi

(3) Kila Mwalimu wa Shule ya Msingi kupewa nyumba ya kuishi ya shule

(4) kuwepo Kituo cha Afya kipya (Zahanati imepanuliwa na kuwa Kituo cha Afya). Tsh 500m (ujenzi) na Tsh 100 (vifaa tiba)

(5) Umemejua (solar) kutumiwa na baadhi ya wakazi wa hapo Kisiwani. Kampuni binafsi inauza umemejua.

Miradi mipya inayotekelezwa:
(5) Sekondari inajengwa kwa nguvu za wananchi na viongozi wao

(6) Umemejua unafungwa kwenye Kituo cha Afya. Huu ni Mradi wa REA wa Tsh 345m

(7) RUWASA itafunga miundombinu ya usambazaji wa maji safi na salama baada ya kuwepo umemejua mwingi na wenye uwezo mkubwa

SHUKRANI:
Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Alhamisi, 12.9.2024