VIJIJI VIWILI VYA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI VYAAMUA KUJENGA SEKONDARI YAO
SHULE YA MSINGI MURANGI – SOMO LA STADI ZA KAZI LATUMIKA KUIMARISHA KILIMO CHA UMWAGILIAJI
BOMBA LA MAJI SAFI NA SALAMA – MRADI WA MUGANGO-KIABAKARI-BUTIAMA
MIRADI YA SEKTA YA AFYA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

baadhi ya MAJENGO ya Hospitali ya Wilaya inayojengwa Jimboni mwetu (Kitongoji cha Kwikonero, Kijiji cha Suguti). DC, DED, MADIWANI na Wafanyakazi wa Halmashauri yetu WAPEWE PONGEZI nyingi sana kwa usimamiaji mzuri wa ujenzi wa Hospitali hii
Jimbo lina Kata 21, Vijiji 68, Vitongoji 374
ZAHANATI
* 24 za Serikali zinazotoa huduma
* 4 za Binafsi zinatoa huduma
* 13 MPYA zimeanza kujengwa na Wanavijiji wakishirikiana na Wadau wa Maendeleo yao
VITUO VYA AFYA
* 2 vya Serikali vinavyotoa huduma za Afya (Murangi & Mugango)
* 1 KIPYA kimeanza kujengwa na Wanavijiji (Kata ya Nyambono) wakishirikiana na Wadau wa Maendeleo yao
HOSPITALI YA WILAYA
* Inajengwa kwenye Kitongoji cha Kwikonero, Kijiji cha Suguti, Kata ya Suguti
* Serikali imetoa Tsh 1.5 bilioni kuanza ujenzi wake
* Kila Kijiji kimekubali kuchangia Tsh Milioni 2.
* Mbunge wa Jimbo amekubali kuchangia
ZAHANATI ZINAZOJENGWA NA WANAVIJIJI
(1) Kitongoji cha Burungu, Kijijini Bukumi, Kata ya Bukumi
(2) Kijijini Butata, Kata ya Bukima
(3) Kijijini Chimati, Kata ya Makojo
(4) Kijijini Chirorwe, Kata ya Suguti
(5) Kijijini Kakisheri, Kata ya Nyakatende
(6) Kijijini Kurwaki, Kata ya Mugango
(7) Kijijini Maneke, Kata ya Busambara
(8) Kijijini Mkirira, Kata ya Nyegina
(9) Kijijini Kurukerege, Kata ya Nyegina
(10) Kijijini Nyegina, Kata ya Nyegina
(11) Kijijini Mmahare, Kata ya Etaro
(12) Kijijini Bwai Kwitururu, Kata ya Kiriba
(13) Kijijini Nyasaungu, Kata ya Ifulifu
WANAFUNZI WA NYAMBONO SECONDARY SCHOOL WAFURAHIA MADAWATI YALIYOTOLEWA NA BENKI YA NMB
UONGEZAJI WA HIGH SCHOOLS NA UBORESHAJI WA ELIMU YA SAYANSI KWENYE SEKONDARI ZETU
WAFUGAJI WAAMUA KUTUMIA MIFUGO YAO KUCHANGIA UJENZI WA SEKONDARI MPYA, ZAHANATI NA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SHULE YA MSINGI
SEKONDARI MOJA YA KATA HAITOSHI – WANANCHI WAAMUA KUJENGA SEKONDARI YA PILI
UKARABATI WA MABWENI YA SEKONDARI YA BWASI
MBEGU YA MIHOGO YA AINA YA MKOMBOZI YANUFAISHA WAKULIMA JIMBONI
HALMASHAURI YASHIRIKIANA NA MRADI WA BMZ (Ujerumani) KUTOA HUDUMA KWA VITUO VYA ELIMU YA WATOTO WENYE ULEMAVU
UJENZI WA SHULE SHIKIZI MWALONI KIJIJINI BURAGA UNAENDELEA VIZURI
WANAKIJIJI NA SERIKALI KUPITIA MRADI WA EQUIP WAKAMILISHA UJENZI WA SHULE SHIKIZI MWIRINGO
MRADI WA USAMBAZAJI WA MAJI WATEKELEZWA KWENYE VIJIJI VITANO (5)
KIKUNDI CHA NGUVUKAZI CHATOA MSAADA WA CHAKULA SHULENI
KILIMO CHA UMWAGILIAJI CHANUFAISHA KIUCHUMI KIKUNDI CHA MKULIMA JEMBE CHA KATA YA BUKIMA
UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA AFYA WAPAMBA MOTO JIMBONI
SERIKALI YASAIDIA SHULE YA MSINGI KIRIBA KWENYE UJENZI WA VYUMBA VIPYA VYA MADARASA NA UPATIKANAJI WA MADAWATI
KIJIJI CHA NYASAUNGU WATUMIA WIKI 1 KUKAMILISHA MSINGI WA SEKONDARI WANAYOIJENGA
SERIKALI YAPIGA JEKI WANAKIJIJI KWENYE KATA YA BUGWEMA KUJENGA SHULE SHIKIZI
ELIMU YA KILIMO SHULENI – SHULE YA SEKONDARI NYANJA YAANZA KUTOA ELIMU YA KILIMO CHA ALIZETI KWA WANAFUNZI WAKE
MKURUGENZI KAYOMBO ATOA MIKOPO YENYE THAMANI YA SHILLINGI MILLIONI 11 KWA VIKUNDI VYA KWIKUBA CARPENTRY NA AMANI NA UPENDO, HALMASHAURI YAFIKIA ASILIMIA 92.6 YA LENGO LA UTOAJI MIKOPO KWA MWAKA WA FEDHA 2018/2019*.
SHEREHE NA MAENDELEO VIJIJINI – KIJIJI CHA NYEGINA CHAAMUA KUJENGA SEKONDARI YAKE
SHEREHE NA MAENDELEO VIJIJINI: KATA YA KIRIBA IMEANZA UJENZI WA MIUNDOMBINU KWENYE SHULE ZAKE KWA KASI MPYA
EID EL FITR NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – SHEREHE NA MAENDELEO VIJIJINI
UKAGUZI WA UJENZI WA HOSPITAL YA WILAYA
SHIRIKA LA BMZ LAENDELEA KUWAWEZESHA WATU WENYE ULEMAVU NA WANAFUNZI WA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
KITONGOJI CHA RWANGA CHAENDELEA KWA KASI KUBWA KUJENGA SHULE YAKE YA MSINGI
WANAKAZI WA KIJIJI CHA KAKISHERI WACHOSHWA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA HUDUMA ZA AFYA
UJENZI WA SHULE SHIKIZI YA KIJIJI CHA BUANGA WAFIKIA HATUA NZURI
DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL – KUANZA KUCHUKUA WANAFUNZI WA FORM I JANUARY 2020
BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL
UJENZI WA ZAHANATI YA KIJIJI CHA MKIRIRA WAENDELEA VIZURI
WAZALIWA WA KATA YA NYAMBONO WATEKELEZA AHADI ZAO KWA VITENDO: JENGO LA OPD LA KITUO CHA AFYA NYAMBONO LAKARIBIA KUEZEKWA
KILIMO CHA UMWAGILIAJI CHAANZA KUWEKEWA MKAZO JIMBONI MWETU
UJENZI WA KITUO CHA AFYA MUGANGO: SERIKALI NA WANANCHI WAENDELEA KUSHIRIKIANA KWENYE UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO
UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA KIJIJINI SUGUTI WAENDELEA VIZURI
WANANCHI WA KIJIJI CHA ETARO WAMEDHAMIRIA KUKAMILISHA UJENZI VYUMBA 5 VYA MADARASA IFIKAPO MWISHONI MWA MEI 2019
UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA YA MRADI WA SERIKALI WA EP4R WATEKELEZWA KIJIJINI CHIRORWE
WANAFUNZI 133 WA FORM I WA SHULE YA SEKONDARI BUKIMA WALIOSUBIRI UPATIKANAJI WA VYUMBA VYA MADARASA WAANZA MASOMO
MAKTABA YAZINDULIWA KISIWANI RUKUBA – ZAWADI YA PASAKA KWA WAKAZI WA KISIWA HICHO
WANANCHI WA KIJIJI CHA KABEGI WAAMUA KUJENGA SHULE SHIKIZI KWENYE KITONGOJI CHA BINYAGO
WANANCHI WA KISIWA CHA RUKUBA WAANZA MAANDALIZI YA UJENZI WA WODI YA MAMA NA WATOTO
WANAVIJIJI WALIKUBALI ZAO JIPYA LA BIASHARA LA ALIZETI JIMBONI MWAO
PAROKIA YA BUKIMA YAJENGA MAABARA YA KISASA YA VIPIMO VYA AFYA
WANANCHI WA KATA YA MUGANGO WAWA MFANO WA KUIGWA KWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO
SERIKALI YATOA SHILINGI MILIONI 146 KWENYE SHULE YA SEKONDARI KIRIBA
UJENZI NA UKAMILISHAJI WA MAABARA KWENYE SEKONDARI ZA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
JIWE LA MSINGI LA “DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL” KUWEKWA TAREHE 18.04.2019
WANANCHI KIJIJI CHA CHIMATI WAAMUA KUJENGA ZAHANATI YA KIJIJI CHAO
UJENZI WA SHULE SHIKIZI BUSAMBARA UMEPATA MSUKUMO MPYA BAADA YA KUSUASUA KWA MIEZI KADHAA
S/M RUKUBA YAKARIBIA KUKAMILISHA UJENZI WA MAKTABA YAO – MFANO WA KUIGWA NA SHULE NYINGINE
UFAULU MDOGO NA UMBALI MKUBWA WA SHULE ZA JIRANI VIMEWAFANYA WAKAZI WA KITONGOJI CHA MWALONI KUAMUA KUJENGA SHULE YAO
JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – UJENZI WA ZAHANATI WAZIDI KUSHIKA KASI JIMBONI
MIRADI YA TANROADS NA TARURA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI YAKAGULIWA
MBUNGE ACHANGIA SARUJI KATIKA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA YA S/M RWANGA.
WANANCHI WA KIJIJI CHA WANYERE WAENDELEA NA UJENZI WA VYUMBA VIPYA VYA MADARASA
WANANCHI WA KIJIJI CHA BUSUNGU WAAMUA KUTOKOMEZA UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SHULE YAO YA MSINGI
KIJIJI CHA KAKISHERI CHAAMUA KUJENGA ZAHANATI YA KIJIJI CHAO
WANANCHI KIJIJI CHA NYABAENGERE WAMEAMUA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU KWENYE SHULE YAO YA MSINGI – KILA KITONGOJI KUJENGA DARASA MOJA
KATA YA BUKIMA WAAMUA KUTATUA TATIZO LA UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MASOMO YA KIDATO CHA KWANZA
UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI MWETU NI WA LAZIMA KUFANYIKA SASA NA KWA KASI KUBWA
WANAFUNZI 232 NDANI YA CHUMBA KIMOJA CHA DARASA – WANANACHI WAAMUA KUTATUA MATATIZO YA UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA MASHULEN
WANAFUNZI WA DARASA LA 7 JIMBONI WANAFAULU LAKINI WANACHAGULIWA WACHACHE KUENDELEA NA MASOMO YA SEKONDARI KUTOKANA NA UPUNGUFU MKUBWA WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SEKONDARI ZA KATA
WANANCHI WA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI WAMEAMUA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI MWAO
MBUNGE WA MUSOMA VIJIJINI AENDELEA KUSHIRIKIANA NA WANAVIJIJI JIMBONI KUJENGA NA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU
KIJIJI CHA BUIRA CHAONYESHA NJIA, CHAJENGA MAKTABA KWENYE SHULE YAKE YA MSINGI
WANAVIJIJI WA KATA YA KIRIBA – WASEMA – “HAKUNA MTOTO ALIYECHAGULIWA KWENDA FORM I ATAKAYEBAKI NYUMBANI KWA SABABU YA UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SEKONDARI YAO YA KATA.”
SHEREHE ZA KRISMASI ZA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI ZIMEFANYIKA KWENYE KANISA LA KATOLIKI KIJIJINI BUKUMI
KATA ZASHINDANA KUJENGA MIUNDOMBINU YA ELIMU NA AFYA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
PROF MUHONGO AOMBA JINA LAKE LIACHWE NA BADALA YAKE LICHUKULIWE JINA LA MAREHEMU JAJI DAN MAPIGANO
WANAFUNZI WAWILI TU WA KUTOKA KITONGOJI CHA BURAGA MWALONI NDIO WAMECHAGULIWA KUENDELEA NA MASOMO YA SEKONDARI – WAZAZI WACHARUKA NA KUAMUA KUJENGA SHULE YAO YA MSINGI
UBORESHAJI WA KILIMO CHA ZAO LA MIHOGO NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
MIUNDOMBINU YA ELIMU – UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
WANANCHI WA KIJIJI CHA CHIMATI WAMEAMUA KUPUNGUZA UHABA WA VYUMBA VYA MADARASA
SHULE SHIKIZI EGENGE YAKAMILIKA
BMZ WAKAMILISHA ZOEZI LA UGAWAJI WA VIFAA VYA ELIMU KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU
UJENZI WA VYUMBA VINNE VYA MADARASA YA SHULE SHIKIZI YA MWIKOKO WAFIKIA HATUA NZURI
PROF MUHONGO ACHANGIA SARUJI SIKU YA MAHAFARI YA SHULE YA SEKONDARI SUGUTI

Prof Sospeter Muhongo amechangia Saruji Mifuko 50 kwenye Harambee ya kuchangia ukamilishaji wa ujenzi wa Jengo la Utawala wa Shule ya Sekondari Suguti.
Na Hamisa Gamba, Msaidizi wa Mbunge
WANANCHI WA KIJIJI CHA BUANGA KUKAMILISHA UJENZI WA SHULE JANUARI 2019
PROF MUHONGO ASHIRIKI HARAMBEE UJENZI WA BWENI LA WASICHANA LA SEKONDARI YA BWASI
VIKUNDI VYA BUSTANI KUTOA FURSA ZAIDI ZA KILIMO CHA UMWAGILIAJI
KILIMO CHA KISASA CHA WANANCHI WENYEWE NDANI YA BONDE LA BUGWEMA
WAZIRI WA NISHATI AKAGUA UTEKELEZAJI WA MRADI WA REA III JIMBONI

Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani akikagua Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini wa REA III ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini
Na Fedson Masawa, Msaidizi wa Mbunge
18 – 09 – 2018
WAZIRI wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amefanya ziara ya Ukaguzi wa Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini wa REA III ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini ambapo pia ametumia fursa hiyo kuzungumza na wananchi wa Jimbo hilo kuhusu masuala mbalimbali yahusuyo Umeme Vijijini.
Akizungumza katika Mkutano wa hadhara leo Agosti 18, 2019 Kijijini Nyakatende, Dkt. Kalemani amewahakikishia wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini kwamba TAASISI, maeneo mbalimbali ya UWEKEZAJI na VITONGOJI vyote 374 vya Jimbo VITAPATA UMEME.
Awali akieleza kuhusu kero ya Umeme Musoma Vijijini, Waziri Kalemani amesisitiza kuwa Prof Muhongo aliomba Umeme kwenye Vijiji vyake vyote 68 na amepewa Vijiji vyote katika Mradi wa REA III
Akisisitiza juu ya jambo hilo, Dkt. Kalemani amesema kuwa kazi ya Mkandarasa ni kuhakikisha anapeleka umeme Vijiji vyote 68 vyenye VITONGOJI 374 katika awamu hii ya REA III
“Hakuna kijiji, hakuna kitongoji na hakuna mwananchi atakayerukwa katika Mradi huu” Amesisitiza Mhe Dkt. Kalemani
Aidha Waziri Dkt Kalemani ametoa maelekezo ya Uboreshaji wa Utekelezaji wa Mradi wa REA III mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Madiwani na WANANCHI wa Musoma Vijijini.
Dkt. Kalemani amewaagiza watendaji wake kufanya kazi bila kuondoka saiti hadi watakapokamilisha kazi hiyo.
“Mkandarasi nataka usihamishe genge, peleka genge kila kijiji. Badala ya kuhamishahamisha,” alisema Waziri wa Nishati Mhe Dkt Kalemani.
Vilevile, Dkt. Kalemani ameshiriki Tukio la Kuwasha Umeme Kijijini Nyakatende kuashiria Uzinduzi rasmi wa Mradi wa REA III Musoma Vijijini.
Katika Ziara yake hiyo, Dkt Kalemani aliongozana viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati na Taasisi zake ambao ni pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu TANESCO, Kaimu Mtendaji Mkuu wa REA, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Mara, Engineer wa TANESCO Kanda ya Ziwa (Mwanza), Engineer wa Miradi ya REA Kutoka Makao Makuu, na Mkandarasi wa Mradi wa REA III Mkoa wa Mara.
Dkt. Kalemani amehitimisha ziara yake Jimboni kwa kutoa pongezi nyingi kwa Mbunge wa Jimbo, Prof Muhongo kwa Jitihada kubwa za Maendeleo anazozifanya. akishirikiana na Mkuu wa Wilaya, Dr. Vicent Naano na Viongozi wengine. Mhe Waziri amewataka Madiwani na Mkurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha Jimbo la Musoma Vijijini linapiga hatua kubwa za kimaendeleo.
KILA KIJIJI KINACHANGIWA KILO 100 ZA MBEGU YA MTAMA.
KIJIJI CHA BUTATA CHAEZEKA CHUMBA KINGINE CHA DARASA KWA KUTUMIA MCHANGO WA FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO
KASI YA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI YAONGEZEKA
KILIMO CHA MAZAO MAPYA YA ALIZETI NA UFUTA CHAFUFUA MATUMAINI YA UCHUMI IMARA JIMBONI
ZAHANATI YA KISIWA CHA RUKUBA YAPATA DARUBINI
Wakazi wa Kisiwa cha Rukuba wanalazimika kusafiri kwa boti na mitumbwi kutoka Kisiwani hadi Musoma Mjini kwenda kufanyiwa VIPIMO VYA MATIBABU kwa sababu Zahanati yao haina DARUBINI.
Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo AMEMWOMBA DAKTARI BINGWA, Dr Derick Davis Nyasebwa wa Uhuru Hospital ya Mwanza
ATOE MSAADA WA DARUBINI MOJA YA KISASA YA KUTUMIWA KUFANYA VIPIMO VYA MATIBABU. Daktari Bingwa huyo amekubali.
DARUBINI hiyo itapelekwa Kisiwani Rukuba hivi karibuni.
Vilevile Mbunge Prof Muhongo ataenda hapo Kisiwani KUZINDUA MAJENGO yaliyojengwa na MFADHILI MKUU (MFARANSA) WA MAENDELEO wa Kisiwa cha Rukuba.
KARIBUNI TUJENGE UCHUMI WA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
DR DERRICK NYASEBWA HONGERA KWA KUTEKELEZA AHADI ZAKO KWA VITENDO.
WANANCHI WA KATA YA RUSOLI WAHAMASIKA NA UJENZI WA MAABARA KWENYE SEKONDARI YA KIJIJINI MWAO

UPAUAJI wa JENGO la MAABARA unaendelea kwenye Shule ya Sekondari Rusoli. Aliyevaa kofia kwenye picha ni Mhe Diwani Boaz Nyeula alipotembelea Maabara ya Sekondari ya Rusoli.
UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI BUSAMBARA WAENDELEA KWA KASI KUBWA

WANANCHI WA KATA YA BUSAMBARA (Vijiji vya Maneke, Kwikuba na Mwiringo) Wakijitolea kusomba mchanga, mawe, kokoto, kufyatua tofali, kusomba maji ili kumsaidia Fundi ujenzi.
SHEREHE ZA UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI NYEGINA B, KIJIJI CHA NYEGINA

Tarehe 15.07.2018, Mbunge Prof Sospeter Muhongo (Mgeni Rasmi) na Viongozi wa Vyama vya Siasa (CCM, CHADEMA, ACT) na Serikali walishiriki Sherehe za Uzinduzi wa S/M Nyegina B.
UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini akishirikiana na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Musoma Vijijini, Ndugu Nyabukika KUHAMASISHA ujenzi wa Vyumba vya Madarasa vya Shule za Msingi na Sekondari Jimboni mwao
Jumamosi, 14.07.2018, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini alishirikiana na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Musoma Vijijini, Ndugu Nyabukika KUHAMASISHA ujenzi wa Vyumba vya Madarasa vya Shule za Msingi na Sekondari Jimboni mwao. Katibu wa CCM Wilaya Ndg Koyo na Mjumbe wa Kamati ya Siasa Ndg Mwalimu Kerenge walishiriki kwenye ziara hiyo ya UHAMASISHAJI wa uboreshaji wa miundombinu ya Elimu kwenye Jimbo la Musoma Vijijini.
(1) SHULE MPYA YA MSINGI YA MWIKOKO, Kijiji cha Chitare, Kata ya Makojo: Picha Namba 1-4 hapo chini zinaonyesha Mkutano wa Wanakijiji wa Chitare wakishiriki HARAMBEE ya kuchangia ujenzi wa Vyumba Vipya vya Madarasa ya Shule hiyo ya Msingi. Kwa awamu hii ya ujenzi, Mbunge Prof Muhongo amechangia Saruji Mifuko 5O iliyonunuliwa Kijiji jirani cha Bukima.
(2) SEKONDARI YA KATA YA USAMBARA: Kata hii yenye Vijiji 3 (Maneke, Kwikuba na Mwiringo) haina Sekondari.
Wananchi wa Kata ya Busambara WAMEAMUA KWAMBA IFIKAPO JANUARI 2019 Sekondari hiyo iwe IMEKAMILIKA na kuanza kutoa elimu.
Wananchi wamepiga HARAMBEE kwa kutoa fedha taslimu na vifaa vya ujenzi. Mbunge Prof Muhongo, amechangia Saruji Mifuko 50 iliyonunuliwa Kijijini hapo. Michango mingine atatoa baada ya KURIDHIKA na KASI ya ushiriki wa Vijiji vya Maneke na Mwiringo kwenye ujenzi wa Sekondari hii. Ushiriki wa Vijiji hivi viwili kwa sasa ni hafifu.
Picha Namba 5-8 zinaonyesha Mkutano wa Wananchi wa Kata ya Busambara wakishiriki kwenye HARAMBEE ya ujenzi wa Sekondari ya Kata yao.
Wananchi wa Vijiji vya CHITARE (Kata ya Makojo), na KWIKUBA, MWIRINGO na MANEKE (Kata ya Busambara) wanaomba MCHANGO WAKO UWASAIDIE ujenzi wa shule zao ambazo WAMEAMUA KUZIJENGA KWA KUJITOLEA na kwa kushirikiana na Serikali.
KILIMO CHA MVUA ZA VULI
JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – TUJITAYARISHE KWA KILIMO CHA MVUA ZA VULI
Wataalamu wetu wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma WANATUSHAURI hivi:
KILIMO cha MTAMA, MIHOGO na MAHINDI cha Msimu wa Vuli huanza mwishoni mwa Mwezi SEPTEMBA, na kuendelea hadi OKTOBA na NOVEMBA.
MBEGU ZINAZOHITAJIKA
Kiasi cha MBEGU kinachohitajika
(1) Mahindi: Kilo 82,500 kwa Ekari 20,625
(2) Mtama: Kilo 21,000 kwa Ekari 7,000
(3) Mihogo: Pingili 78,000,000 kwa Ekari 19,500
BEI ZA MBEGU (ASA MOROGORO)
(1) Mtama: Tshs 2,300 kwa kilo moja
(2) Mahindi: Tshs 2, 300 kwa kilo moja
(3) Vijiti Vya Mihogo: Tshs 200,000 vinavyotosha ekari moja
Ndugu zangu MADIWANI, HALMASHAURI, MKUU WA WILAYA, MBUNGE wa JIMBO, na WADAU wa MAENDELEO YA MUSOMA VIJIJINI tunaombwa tujitayarishe KUZIPATA MBEGU HIZI KWA WAKULIMA JIMBONI KWENYE MWEZI AGOSTI 2018 (mbegu kuanza kugawiwa Jimboni katikati mwa Agosti 2018).
Nashauri tufanye Kikao tarehe 10 Julai 2018 Ofisini kwa DC wa Musoma kujadili na kuweka bayana namna ya kuzipata mbegu hizo.
Je Wanavijiji wauziwe mbegu au Wanavijiji wapewe mkopo wa mbegu hizo au Wanavijiji wasaidiwe kwa kugawiwa mbegu hizo bure kutokana na uchumi wao kuwa hafifu.
WANANCHI WAMEKUA NA MWITIKIO MKUBWA WA KUJITUMA NA KUJITOLEA KUHARAKISHA UPATIKANAJI WA MAENDELEO YAO

Mbunge wa Musoma Vijijini, akifuatana wa Viongozi wa Wilaya wa CCM (Katibu wa CCM, Katibu wa WAZAZI na Katibu wa UVCCM) kukagua MIRADI YA UJENZI inayotekelezwa Jimboni humo.
Jumatano, 13.06.2018, Mbunge wa Musoma Vijijini, akifuatana wa Viongozi wa Wilaya wa CCM (Katibu wa CCM, Katibu wa WAZAZI na Katibu wa UVCCM) wamekagua MIRADI YA UJENZI inayotekelezwa Jimboni humo kwa wakati huu.
Kijiji cha Bukima kimeamua KUPANUA ZAHANATI YAKE kwa kuongeza Jengo lenye WADI 3 (Wadi ya Wazazi, Watoto & Akina Mama, na Wadi ya Wanaume). Picha za kwanza 3 zinaonyesha eneo la ujenzi huo. Mbunge wa Musoma Vijijini amechangia Saruji Mifuko 100 na wananchi wanaendelea kuchangia saruji, kusomba mawe, mchanga, n.k.
Kijiji cha Saragana wameamua kujenga KITUO CHA POLISI kitakachohudumia Kata zaidi ya 2. Wananchi wamejitolea kusomba mchanga na maji ya kufyatua tofali zaidi ya 4,000. Polisi Wilaya (OCD) imechangia Saruji Mifuko 60 na leo Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter amechangia Saruji Mifuko 100. Picha namba 4 na 5 hapo chini zinaonyesha tukio hilo Kijijini Saragana.
Kijiji cha Nyambono kimekubali KUSHIRIKIANA na Wazaliwa wa Kijiji hicho (Wafadhili) kujenga KITUO CHA AFYA. Wiki hii wanamaliza ujenzi wa msingi wa Jengo la Matibabu. Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo amechangia Saruji Mifuko 100. Picha 2 za mwisho zinaonyesha msingi unaojengwa.
Wananchi wa Vijiji vyote 68 vya Jimbo la Musoma Vijijini wamekuwa na hamasa ya KUJITOLEA kuharakisha Ujenzi na Uboreshaji wa Miundombinu ya Elimu na Afya vijijini mwao kwa kushirikiana na Serikali.
UJENZI WA ZAHANATI VIJIJINI KWA NJIA YA KUJITOLEA WAPAMBA MOTO

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Sospeter Muhongo akikagua ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Kigera Etuma
Na Fedson Masawa, Msaidizi wa Mbunge
Ujenzi wa zahanati umezidi kupamba moto katika vijiji mbalimbali vya vya Jimbo la Musoma Vijijini ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (2015-2020).
Hatua hiyo imefikiwa ikiwa ni matokeo ya hamasa kubwa kutoka kwa wananchi wa Musoma Vijijini walioamua kuungana na serikali, viongozi wao na wadau mbalimbali wa maendeleo ili kusogeza huduma ya afya kwa kila kijiji Jimboni humo.
Awali akiungana na wananchi, viongozi na wadau mbalimbali wa maendeleo Jimboni mwake Mei 1, 2018, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Sospeter Muhongo alishirikiana na Madiwani na wakazi wa kijiji cha Kurwaki na kijiji cha Kigera Etuma na kufanikiwa kuchangia zaidi ya mifuko 350 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Kurwaki kata ya Mugango na mifuko 150, nondo na misumali katika zahanati ya Kigera Etuma kata ya Nyakatende.
Akitoa taarifa ya ujenzi wa zahanati ya Kigera Etuma, mtendaji wa kijiji hicho ndugu Antony Ndege alisema, wachangiaji wa ujenzi wa Kijiji cha Kigera Etuma ni Wafadhili,Halmshauripamoja na wakazi wa kijiji hicho na tayari jengo la matibabu (OPD) limekamilika kwa asilimia 80 na nyumba ya Mganga na Muuguzi (two in one) inajengwa kwa kasi kubwa.
Mtendaji ameongezea kuwa “malengo ya wananchi na serikali ya kijiji cha Kigera Etuma ni kukamilisha ujenzi huo mapema ifikapo Desemba 2018 zahanati hiyo iwe imeanza kazi”
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Musoma na Diwani wa kata ya Mugango Mhe Charles Magoma kwa niaba ya wananchi amemshukuru Mbunge na wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini kwa kuungana kufanimisha miundombinu ya Elimj, Afya na Kilimo Jimboni.
MABARAZA YA WAZEE WA USHAURI, USHAWISHI NA MAADILI
Na Fedson Masawa, Msaidizi wa Mbunge
PROF. MUHONGO AZINDUA MABARAZA YA WAZEE WA USHAURI, USHAWISHI NA MAADILI

Wazee wa mabaraza ya kata 21 za jimbo la Musoma vijijini wakiwa kwenye kikao cha uzinduzi wa mabaraza yao uliotekelezwa na Mbunge wa Jimbo holi Prof. Muhongo (hayupo katika picha)
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Sospeter Muhongo leo April 30 amefanya uzinduzi wa mabaraza ya wazee wa ushauri na maadili ngazi ya kata kwa kata zote 21 za Jimbo hilo.
Akizungumza na wazee wakati wa uzinduzi wa mabaraza hayo kijijini Chumwi, Prof Muhongo amewaeleza wazee hao kuwa majukumu yao makubwa ni kutoa ushauri na kuhamasisha shughuli za maendeeo bila kuingilia miimili ya serikali za vijiji, kata n.k ili kuharakisha mafanikio chanya Jimboni.
Kwa upande wao wazee kutoka kata 21 za Jimbo la Musom vijijini wameungana pamoja kuhakikisha wanasimamia majukumu yao ya ushawishi, ushauri na uhamasishi katika mendeleo na uchumi hasa Elimu, Afya na Kilimo vikiwa ni vipaumbele vya Jimbohilo.
“Tutahakikisha Elimu, Afya na Kilimo ndio itakuwa nguzo ya kuinua uchumi na maendeleo ya Jimbo letu” alisema mzee Chriphod Nyaturo kwa niaba ya wazee wa hao.
Hii ni mara ya pili Prof Muhongo akizindua mabaraza ya wazee ambapo kwa mara ya kwanza alizindua mabaraza ya wazee ngazi ya vijiji mwishoni mwa mwezi Machi 2018, lengo likiwa ni kuimarisha nguvu ya ushawishi na uhamasishaji wa shughuli za maendeleo na uchumi Jimboni.
Kwa upande mwingine, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini amefanya Kikao na Wenyeviti wa CCM wa Kata za Jimbo lake wakijadili juu ya usimamiaji wao wa utekelezaji wa Miradi ya Uchumi na Maendeleo (Ilani ya CCM ya Uchaguzi) kwenye Kata zao.
WANAWAKE WATAKIWA KUUNDA VIKUNDI VYA MAENDELEO
Na Hamisa Gamba
MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi CCM (UWT) Mkoani Mara, Wegesa Hassan amewataka wanawake mkoani humo kuunda vikundi ili kufanya miradi mbalimbali itakayowaletea maendeleo.
Wegesa alitoa wito huo kwenye kikao cha Jumuiya hiyo kilichofanyika Murangi, kwa lengo la kuhamasisha mshikamano na suala la maendeleo, ambapo aliwataka wanawake kuachana na makundi yasiyo na tija ndani ya Jumuiya yao.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT Musoma vijijini Abia Masaule kwa niaba ya wajumbe wake, ametoa shukrani kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma vijijini Prof. Sospeter Muhongo kwa umoja alioonesha na kuungana na wanawake hao katika kuwezesha kikao hicho kilichofanyika Machi 21, 2018.
MBUNGE MUSOMA VIJIJINI AWATEMBELEA WAHANGA WA KIMBUNGA

Mbunge wa Jimbo la Musoma vijijini Prof. Sospeter Muhongo (katikati aliyevaa fulana ya bluu) akiwa katika shule ya msingi Bukumi ambapo vyumba vitatu vya madarasa paa zake zimeezuliwa na upepo mkali ulioambatana na mvua. Kulia kwake ni Diwani wa viti maalum kata ya Mgango Kadogo Kapi wakiwa na Diwani wa Kata ya Bukumi John Manyama.
Na Verdiana Mgoma
MBUNGE wa Jimbo la Musoma vijijini Prof. Sospeter Muhongo amezitembelea kaya zilizopatwa na matatizo ya nyumba zao kuezuliwa na upepo na nyingine kubomoka kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali Jimboni humo.
Kwenye ziara yake aliyoianza Machi 15, 2018, Prof. Muhongo ameshuhudia kaya 86 zikiwa zimekumbwa na matatizo hayo na kusababisha baadhi ya familia kukosa makazi.
Mbali na kutembelea kaya hizo na kutoa pole, mbunge huyo alitembelea shule ya msingi Bukumi iliyopo kijiji cha Bukumi ambapo ameshuhudia vyumba vitatu vya madarasa paa zake zikiwa zimeezuliwa na upepo na mashamba ya pamba yenye takribani hekari 200 yaliyoharibiwa vibaya na mvua ya mawe katika kijiji cha Bugwema.
Akizungumza na wananchi waliokumbwa na matatizo hayo, Prof. Muhongo amewataka kuwa watulivu wakati viongozi wakiendelea kufanya tathimini ya uharibifu uliotokea na kuwasihi wasitegemee msaada kutoka serikalini peke yake kwani suala hilo ni la jamii nzima kwa kushirikiana na serikali.
“Kuweni wavumilivu, viongozi na wasaidizi wangu watapita na kuchukua tathimini ya madhara yaliyotokea. Pia tambueni, serikali peke yake haiwezi kutoa msaada kwa kila mtu. Kilichopo ni ninyi wananchi na sisi kujipanga tuone tutalitatuaje hili” alisema Prof Muhongo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi wa maeneo yaliyopata tatizo hilo mbali na kusikitishwa na matukio hayo yanayojirudia kila mara, walimpongeza mbunge wao na uongozi wa Halmashauri ya Musoma kwa kuwatembelea na kuwapa pole.
“Tunamshukuru sana Prof. Muhongo na viongozi wenzake wa halmashauri kwa kuguswa na kutufikia wananchi wao kwa wakati hasa tunapopatwa na matatizo ya aina hiyo” alisema Furaha Sumuni.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Musoma Charles Magoma alisema, ili kupunguza matatizo ya mara kwa mara, wameshaagiza kila kaya kupanda miti 40, shule miti 500 na zahanati miti 100 kwa kila mwaka huku akikazia kuwa zoezi hilo ni la lazima.